Friday, January 13, 2012

NIMEKWAMBIA NENDA KAUNGE MBOGA...... USIKII...?

ABOUT MY COMPANY'S WEBSITE

"21 Century real estates &Autos Limited" is a real estate and Automobile dealer development company Selling truly affordable and quality houses/Land/Cars for the masses through its " 21 Century real estates &Autos " innovative program and line of products. "

We sale affordable houses/land and cars using adverts i.e Magazine,Newspaper,Blogs and Website and labor to deliver double impact in terms of development to the communities we serve and live in. We use typical Adverts as we mentioned above.  21 Century real estates &Autos 's talented and multi-disciplinary team has combined innovative skills with advanced knowledge's to sale affordable houses/land and cars to all income levels in Tanzania. Our dream "Affordable selling prices" will be achieved when the dreams harbored by millions of people becomes a reality.  21 Century real estates &Autos  is a private limited liability company registered under the companies' ordinance of the United Republic of Tanzania.

TANGAZO

Tangazo


Kwa wale wote ambao wanatafuta Nyumba za kupanga au Kununua,au Viwanja vya kununua au Kuuza.
Pia kama una Gari au Magari unataka kuuza au Kununua basi naomba tuwasiliane na mimi.


Biashara hiyo inafanyika ndani ya kampuni yangu iliyopo maeneno ya Kijitonyama inayojulikana kwa jina la;


21Century real estates& Autos.
Phone;0657011119
Email.m.baitani@yahoo.com

Wednesday, January 11, 2012

BREASTFED BABIES'ARE MORE CRANKY AND CRY MORE'



New mums should be advised that it is normal for their baby to cry more if they are breastfed, say experts.
The Medical Research Council team says this irritability is natural, and although formula-fed babies may appear more content and be easier to pacify, breast is still best.
If parents have more realistic expectations more may stick with breastfeeding, they hope.
Most UK mums try to breastfeed. Within months the rate drops to a third.
The Department of Health recommends that mothers exclusively breastfeed for the first six months after birth.
The most common reason given for women to stop breastfeeding is that "Breast milk alone didn't satisfy my baby", which the MRC scientists say reflects their perception of irritability as a negative signal.

IDARA YA UHAMIAJI YAKAMATA MTANDAO WA BIASHARA YA BINADAMU



Idara ya uhamiaji nchini Tanzania imeendesha msako maalumu na kufanikiwa kukamata mtandao unaojishughulisha na biashara haramu ya binadamu unaoongozwa na mtu aitwaye Ashok Nepal raia Bangladesh.
Naibu kamishna wa Uhamiaji, Bi. Grace Hokororo amesema kuwa katika operesheni hiyo jumla ya watu kumi na sita wamekamatwa wakiwemo raia kutoka nchi za Pakistani, Nepal na Kenya.
Kwa mujibu wa Bi. Hokororo, Ashok anatuhumiwa kuwaingiza chini isivyo halali watu hao na baadaye kuwatafutia viza kwenda nchini Afrika Kusini kwa malipo ya dola za Marekani elfu tano au dawa za kulevya zenye thamani hiyo hiyo ya fedha.

MWANAMKE AFA AKIJARIBU KUOKOA SIMU YAKE!!

Charlene Pickering



Mwanamama mmoja nchini Uingereza amekufa kwa kugogwa na treni ya mwendo kasi baada ya kuruka kwenye mabehewa ili kuiokoa simu yake.
Mwanamama huyo Charlene Pickering,mwenye miaka 23 alikuwa akigombana na mpenzi wake Daniel Pickett wakati alipoiangusha simu hiyo na kujigonga mara nyingi kabla kuangukia kwenye mabehewa.
Mpenzi wake Bw. Pickett alimuomba kurudi katika ghorofa walipokuwa wamesimama lakini ombi lake hilo lilichelewa sana baada ya mwanamke huyo kugongwa na treni ya mwendo aksi inayosafiri mita 60.
Bi. Pickering,anayetoka Magharibi mwa mji wa Molesey, Surrey, ametangazwa kufa katika ajali hiyo kufuatia tukio ilitokea kituo cha Wimbledon kusini magharibi mwa London.

HATIMAYE DUDE AMSAKA NDIKUMANA





SAKATA la minong’ono na madai ya kuwa mtoto wa wanandoa, Irene Uwoya na Hamad Ndikumana ‘Kataut’, ni wa staa wa filamu Bongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’,  limechukua sura mpya baada ya Dude kuibuka na kusema: “Namsaka Ndikumana.”


Akizungumza na Risasi Mchanganyiko katika mahojiano maalum wikiendi iliyopita jijini Dar es Salaam, Dude alisema anamtafuta Ndikumana usiku na mchana ili amweleze ukweli anaoujua tofauti na uvumi uliozagaa kuwa anahusika na mtoto wa Uwoya.
ANAMSAKA USIKU NA MCHANA
Alisema, kwa muda mrefu imekuwa ikienezwa kwamba mtoto wa wanandoa hao ni wake, jambo ambalo si la kweli kwa vile hajawahi kutoka na Uwoya hata siku moja.
“Uwoya ni msanii mwenzangu, kwa maneno mengine Ndiku ni shemeji yangu. Sijawahi kutembea naye (Uwoya) na siwezi kutoka na mke wa mtu.
“Haya mambo yanakuzwa, naishi kwa wasiwasi. Sina amani. Sijui Ndiku anafikiria nini kichwani mwake, ndiyo maana nimeona si vibaya nikamtafuta ili nizungumze naye kiume.
“Hili si jambo la kulikalia kimya. Kwa kweli linanisumbua sana akilini mwangu. Namsaka usiku na mchana. Nataka kuzungumza naye ili kuondoa utata.”

APATA KIGUGUMIZI
Hata hivyo, Dude alipotakiwa kueleza ukweli alionao ambao anataka kumweleza Ndiku, aligoma kueleza chochote kwa madai kuwa anachotaka kukisema kinamhusu Ndiku pekee.
“Siwezi kuzungumza chochote, hata nikisema haitasaidia kitu. Natakiwa kukutana na Ndiku mwenyewe. Yeye ndiye anayetakiwa kuambiwa na mimi. Si mtu mwingine yeyote.
“Kama nilivyokuambia awali, haya mambo yanakuzwa. Si ya kuyakalia kimya... naujua ukweli wa hili suala lakini natakiwa kuzungumza naye tu,” alisema Dude na kuongeza:
“Naamini hatakataa wito wangu... nakumbuka hata kwenye birthday ya Uwoya, nilimwita pembeni nikazungumza naye, ingawa sikuweza kuongea naye suala la mtoto kwa vile watu wengi walikuwa wakimvuta na kuongea naye.”
Akaongeza: “Nilimwambia nitamtafuta muda mwingine...naona ndiyo muda wa kuweka sawa kuhusu suala la mtoto ambalo linazua mjadala mkubwa nikitajwa kuhusika. Nitazungumza naye ndani ya siku mbili tatu hizi, mambo yatakuwa sawa.”



AGOMEA DNA
Katika hali ya kushangaza, pamoja na kwamba Dude alimhakikishia mwandishi wetu kuwa hahusiki kwa namna yoyote na mtoto wa wanandoa hao, lakini alipoulizwa kama atakuwa tayari kuchukuliwa kipimo cha vinasaba (DNA) na mtoto huyo, aligoma.
“Nini, DNA? Kwa nini nipime sasa wakati nimeshasema sihusiki? Kiukweli kuhusu hilo, hata nikiwekewa mtutu wa bunduki mbele yangu, sipimi,” alisema na kuongeza:
“Kupima maana yake ninaungana mkono na hao wanaosambaza hizi taarifa. Ninachojua mimi ni kuwa sijawahi kutembea na Uwoya, hiyo inatosha, kama hawaamini basi!”

MASTAA WANENA MAZITO
Wakati huohuo, BRIGHTON MASALU anaripoti jinsi mastaa wa filamu Bongo walivyotoa maneno mazito, katika mjadala usio rasmi juu ya mgawanyiko wa ndoa hiyo.
 Wakizungumza kwa staili ya kushambulia, mbele ya mwandishi wetu hivi karibuni, Sinza-Mori, Dar, mastaa hao, Vincent Kigosi ‘Ray’, Jacob Steven ‘JB’, Blandina Chagula ‘Johari’ na Steven Mangere ‘Nyerere’, walieleza mitazamo yao juu ya mtafaruku wa ndoa hiyo.

RAY
“Ndikumana ni mkimya lakini ana matatizo. Nilimwambia kabla kuwa anataka kukurupuka, baadhi ya wanawake si wa kuolewa, lakini hakusikia. Hata hivyo ana ukorofi wake (Ndiku), hapendi kusikiliza ushauri na kibaya zaidi ana wivu kupindukia.”

JB
“Nahisi Uwoya hampendi Ndikumana, kampotezea muda wake... huyo mwanamke atateseka sana. Na mimi nadhani kuna kitu ambacho sisi hatukijui, ipo siku kitajulikana lakini Uwoya ana makosa sana hasa aliposema hajawahi kumpenda mumewe. Hata kama ni mimi ningeumia.”

JOHARI
“Jamani nyie hamjui tu, anayoyaona Uwoya kwenye ndoa yake ni ya kutisha. Simtetei kwa kuwa ni rafiki yangu lakini najaribu kukumbuka aliyoniambia, kama ni kweli ni halali waachane kuepusha mengi. Ndikumana ana matatizo,” alisema bila kufafanua zaidi.

STEVE NYERERE
“Hivi mwanaume na akili zangu naweza kuoa mwanamke kama Uwoya? Si nitakuwa najichimbia kaburi langu mwenyewe? Nakumbuka siku moja Uwoya alipanda taxi, Ndikumana akawa anamzuia na baada ya kuondoka jamaa akaanza kulia,” alisema Steve Nyerere, ambapo Ray aliunga mkono kauli hiyo.

KALAMU YA MHARIRI
Ndoa ni muunganiko mtakatifu, pamoja na mzozo uliopo kati ya wanandoa hao, bado wanayo nafasi ya kukaa na kuyamaliza. Familia zao zikitumia nafasi yao vizuri, zinaweza kurejesha amani katika uhusiano wao.

MZEE KIPARA AFARIKI DUNIA!!


Hayati Mzee Kipara


Taarifa zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa mwigizaji mkongwe nchini Tanzania aliyewahi kutamba na kundi la Kaole Fundi Saidi maarufu kama Mzee Kipara amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Akithibitisha taarifa hizo mwigizaji mkongwe Swebe amesema mzee Kipara amefariki leo saa mbili asubuhi akiwa nyumbani Kwake Kigogo jijini Dar es salaam ambapo mpaka anatufikisha taarifa hizi Swebe ndiye aliyekuwa na maiti ya mzee Kipara ndani akifanya jitihada za kuipeleka maiti hiyo Muhimbili.



Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi,Ameen!

Habari kwa Hisani ya Zembwela na Michael Baruti. 

Hamad Rashid awabana CUF Mahakama Kuu Dar

Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed



James Magai na Aziza Masoud
MBUNGE  wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed na wenzake 10 sasa wameiomba Mahakama Kuu Dar es Salaam iiamuru Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Wananchi(CUF) wajieleze ni kwa nini wasitiwe hatiani kwa kukiuka amri ya mahakama hiyo.
Ukiacha wadhamini hao, jana Hamad Rashid  na wenzake, waliomba mahakama iamuru pia wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi wa chama hicho akiwemo Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, Seif Sharrif Hamad wajieleze kwanini wasitiwe hatiani kwa kukiuka amri hiyo.

Pia wanaiomba mahakama hiyo ibatilishe uamuzi wa Baraza Kuu la Uongozi la  chama hicho wa kuwavua uanachama hapo Januari 4, 2012, kwa madai kwamba walikiuka katiba ya CUF.

Kabla ya uamuzi huo wa kuwavua uanachama, Januari 3, 2012, Hamad Rashid na wenzake waliwasilisha ombi  Mahakama Kuu Dar es Salaama chini ya hati ya dharura wakiomba mkutano wa Baraza Kuu la chama hicho uliokuwa ukitarajiwa kufanyika Zanziba, uzuiwe kuwajadili.
Kupitia kwa mawakili wao, kampuni ya uwakili ya GF Law Chambers Advocates  walidai baraza hilo lina nia ya ama kuwasimamisha au kuwavua uanachama na kwamba uamuzi huo ungeathiri haki zao za kikatiba.

Waliendelea kudai kwamba, kuna kesi ya msingi ya madai namba 1 ya mwaka 2012  waliyoifungua mahakamani hapo wakihoji muundo wa Kamati ya Nidhamu na Maadili ya chama hicho   na uteuzi wa wajumbe wa kamati hiyo.
Tayari Jaji Augustine Shangwa katika uamuzi wake wa Januari 4, 2012, aliamuru CUF kusitisha uamuzi wa ama kuwasimamisa au kuwavua uanachama walalamikaji hao.

Hamad Rashid jana alirejea amri hiyo ya mahakama kuu chini ya Jaji  na kueleza kwamba  CUF waliikaidi na badala yake kuendelea na kutekeleza azma yake ya kuwavua uanachama.


Katika hati ya kiapo cha Hamad iliyowasilishwa mahakamani hapo, alidai  kwamba baada ya mahakama kutoa uamuzi huo, wakili wake akisaidina na mtumishi wa mahakama aliyemtaja kwa jina la Khatibu, waliwasilisha taarifa ya amri hiyo ya mahakama katika ofisi za chama hicho Buguruni saa 6:20 mchana.

Hata hivyo alidai kuwa Ofisa wa chama hicho aliyejulikana kwa jina la Mikidadi Nyandula alikataa kuipokea.
Alidai kwamba,  baadaye saa 6:50 wakili wake alimtumia uamuzi wa mahakama hiyo kwa njia ya baruapepe na kwamba yeye Hamad Rashid aliiwasilisha nakala ya uamuzi huo wa mahakama kwa Afisa Mkuu wa mlalamikiwa saa 8.15 mchama ili aiwasilishe kwa Katibu Mkuu.

Hamad Rashid alizidi kudai katika hati hiyo kwamba,  baada ya kuwasilisha uamuzi huo alitakiwa kufika mbele ya Baraza Kuu saa 8:25  na kutakiwa kujitetea na kwamba, ombi lake la muda wa kuandaa utetezi lilikataliwa.
Alisema pia  aliwaarifu wajumbe wa baraza hilo kwamba mahakama kuu ilikuwa imetoa uamuzi na amri ya kulizuia kuendelea na azma yake.

“Niliwaonesha wajumbe wa baraza hilo waliokuwepo katika mkutano huo nakala ya uamuzi huo,” alisisitiza Hamad Rashid katika kiapo chake hicho.

Alifafanua kwamba  hata hivyo, baraza hilo lilipuuza amri hiyo ya mahakama na kusisitiza kuwa ni lazima achague ama kujitetea mwenyewe au kutoka nje ya mkutano. 

“Niliamua kutoka nje ya mkutano ili nisihusike katika kuidharau mahakama,”alifafanua Hamad  Rashid.
Aliendelea kudai kwamba walalamikaji wengine nao waliitwa mbele ya baraza hilo na kila mmoja aliliambia baraza hilo kuwa hawezi kuendelea kwa kuwa kuna amri ya mahakama, ambayo inazuia kuendele na mkutano huo.

“Hivyo, kila mlalamikaji aliwaonesha wajumbe wa baraza hilo nakala ya uamuzi wa mahakama na  lakini wajumbe wa baraza hilo walipuuza na kusisitiza kuwa ni lazima wajitete na walalamikaji waliamua kutoka nje ya mkutano,” alidai Rashid. 
Alidai kwamba siku hiyo hiyo kabla ya uamuzi wa kuwafukuza, wakili wake  aliyemtaja kwa jina moja la Panya mnamo saa 9:05 mchana,  aliwasilisha nakala ya uamuzi huo wa mahakama ofisi ya  makao makuu ya chama hicho Zanzibar.

Aliongeza kuwa licha ya kuwasilisha taarifa hizo kwa wakati katika ofisi za chama hicho na kwa Katibu Mkuu na katika mkutano huo wa baraza kuu, baraza hilo liliendelea na azma yake ambayo hatima yake ilikuwa ni kuwafukuza uanachama wa chama hicho.
“Hatua ya  wa walalamikiwa kuendelea na mkakati wao wa kuwafukuza uanachama walalamikaji ulifanyika saa 9:55 jioni, wakati tayari kulikuwa na amri ya mahakama iliyokuwa imeshawasilishwa kwa walalamikiwa,” alizidi kudai.

Katika hati ya dharura iliyoambatanishwa kwenye maombi yao hayo, walalamikaji hao wanadai kuwa kwa kuzingatia uamuzi huo usio halali, walalamikaji wamewasilisha barua kumfukuza uanachama Rashid kwa Spika wa Bunge kwa ajili ya utekelezaji.
Wanadai kuwa ikiwa Bunge litatekeleza jukumu lake wapiga kura wa jimbo la  Wawi, ambao mbunge wao ni mlalamikaji wa kwanza wanaelekea kunyimwa haki yao ya uwakilishi bungeni.

Mbali na Hamad Rashid wengine waliofukuzwa uanachama CUF ni Doyo Hassan Doyo, Shoka Khamis Juma na Juma Saanane, wote wakiwa wajumbe wa Baraza Kuu la chama hicho.

Yamemkuta tena,Kafulila atiwa mbaroni Kigoma

Anthony Kayanda, Kigoma
POLISI mkoani Kigoma  wamelazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya mamia ya wafuasi wa chama cha NCCR Mageuzi waliokuwa kwenye mkutano ambao ulipaswa kuhutubiwa na mbunge  Kigoma Kusini, David Kafulila.

Habari zilizolifikia gazeti hili zimeeleza kuwa tukio hilo lilitokea juzi katika Kijiji cha Kazuramimba ambako Kafulila alikuwa amejiandaa kufanya  mkutano wa hadhara na tayari alikuwa ameanza kuhutubia akiwa kwenye gari na madiwani wawili wa chama hicho cha upinzani.


Kafulila aliliambia gazeti hili jana kuwa polisi hao walizuia mkutano wake na kumkamata kwa mahojiano yaliyodumu kwa takriban dakika 30, kwa madai kwamba mkutano wake haukufuata taratibu za kuomba na kupata kibali.


Kafulila ambaye yuko mkoani Kigoma kwa ziara ya kichama, alisema alipofika kijijini hapo alipata taarifa kwamba polisi wa kituo kidogo kilichopo eneo hilo waliwazuia viongozi wa NCCR Mageuzi kufanya maandalizi ya mkutano huo.


Alisema baada ya kusikia uamuzi huo, alilazimisha wafanye mkutano kwa vile yeye ni mbunge halali wa jimbo hilo la Kigoma Kusini na anapaswa kuzungumza na wananchi kuelezea utendaji wake wa kazi kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita.


“Polisi wamenizuia kufanya mkutano wangu na wametumia nguvu kubwa kututawanya kwa madai kwamba wametumwa na Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kigoma (OCD), Japhet Kibona eti sisi hatujatimiza masharti..., na pia hatujaomba kibali cha kufanya mkutano. Sasa mimi kama mbunge wa jimbo nazuiliwa kwa nini?," alihoji Kafulila na kuendelea:


"Inawezekana huyu OCD ananihujumu na tayari nimewaeleza wakuu wake wa kazi kuanzia IGP,  Said Mwema na Waziri wa Mambo ya ndani, Shamsi Vuai Nahodha ili wajue hujuma ninayofanyiwa na huyu OCD wa Kigoma,"alisisitiza Kafulila.
Kafulila ambaye hatma ya ubunge wake iko mikononi mwa Mahakama baada ya kuvuliwa uanachama wa NCCR-Mageuzi, alisema katika sakata hilo walikuwepo polisi watano waliovurumisha mabomu ya machozi.


Alisema yeye alikamatwa na kupelekwa kituo kidogo cha Polisi Kazuramimba kwa mahojiano yaliyodumu kwa zaidi ya nusu saa, kabla ya kuachiwa huru kwa sharti la kutoendelea na mkutano wa hadhara.


Alisema kuzuiwa mikutano yake kulianzia Kijiji cha Ilagala ambako hata hivyo anaeleza kuwa mkutano ulifanyika kwa busara za Kamanda wa Polisi mkoa wa Kigoma, ACP Frasser Kashai baada ya kuwa umezuiliwa na askari wa Kituo kidogo cha Polisi Ilagala. 


RPC Kigoma
RPC Kashai alipoulizwa kuhusu suala hilo, alisema kilichotokea ni mbunge huyo kukaidi na kukiuka utaratibu wa kisheria katika kufanya mikutano yake ya hadhara, ambayo ni pamoja na kutoa taarifa ya maandishi polisi ili waweze kuandaa ulinzi.

"Sheria inatamka wazi kwamba, lazima wanaofanya mkutano watoe taarifa polisi kupitia kwa OCD saa 24 kabla, ili na sisi tujipange kwa ajili ya kuweka usalama unakuwepo, sambamba na kujiridhisha kama hakuna mkutano mwingine unaofanyika katika eneo wanalokusudia kufanya mkutano wao," alisema Kamanda Kashai.

Hata hivyo, alikanusha kutokea vurugu zozote katika mkutano huo bali ni kitendo cha polisi kuwazuia wananchi wasihudhurie kutokana na utaratibu kukiukwa, jambo ambalo haliwezi kuvumiliwa na Polisi.
"Kafulila anafanya mambo ya ajabu sana kwa sababu siamini kwamba, hajui sheria na utaratibu wa kufanya mikutano ya hadhara, yeye ana tabia ya kuleta barua siku hiyo hiyo ya mkutano, lakini sheria inaeleza bayana ni lazima taarifa iletwe saa 24 kabla," alisisitiza Kashai.

Alisema hadi jana hakuwa amepata  taarifa zozote za kuwepo kwa watu waliojeruhiwa katika tukio hilo, hali inayoashiria  kwamba hapakutokea vurugu zozote.

Kafulia livuliwa wadhifa wa ukatibu mwenezi wa NCCR Mageuzi, tukio lililofuatiwa na kuvuliwa uanachama katika kikao cha Halmashauri Kuu ya chama hicho kilichofanyika Desemba 17, mwaka jana.


Mbunge huyo alikuwa akituhumiwa kuratibu mpango wa mapinduzi dhidi ya mwenyekiti James Mbatia, pia kukiuka taratibu na katiba ya chama kwa kuzungumza baadhi ya mambo nje ya vikao vya chama.


Uamuzi huo ulikuwa unampotezea ubunge wake lakini, alikimbilia mahakamani kufungua kesi ya msingi kupinga uamuzi huo huku pia akiomba pingamizi la mahakama dhidi ya uongozi wa NCCR-Mageuzi, kuuzuia usitekeleze kitu chochote hadi kesi hiyo ya msingi itakapomaliza.   

MAJAMBOZI......?

Men discovered COLOURS and invented PAINT, Women discovered PAINT and invented MAKEUP.

Men discovered the WORD and invented CONVERSATION, Women discovered CONVERSATION and invented GOSSIP.

Men discovered GAMBLING and invented CARDS, Women discovered CARDS and invented WITCHERY.

Men discovered AGRICULTURE and invented FOOD, Women discovered FOOD and invented DIET.

Men discovered FRIENDSHIP and invented LOVE, Women discovered LOVE and invented MARRIAGE.

Men discovered TRADING and invented MONEY, Women discovered MONEY and invented SHOPPING.

Thereafter Men have discovered and invented a lot of things… While Women STUCK to shopping

IKO KAZI

MPE RUNGU

Tuesday, January 10, 2012

MWANAMUZIKI WA SENEGAL YOUSSOU NDOUR KUWANIA URAIS


Mwanamuziki mashuhuri nchini Senegal na mwanaharakati wa kisiasa,Youssou N'dour, ametangaza kuwa atawania kiti cha urais katika uchaguzi wa mwezi Februari nchini humo.
Mwanamuziki huyo amesema kuwa anaitikia wito wa kumtaka agombee kiti hicho dhidi ya rais wa sasa Abdoulaye Wade, ambaye anapania kuwania kiti hicho kwa muhula wa tatu.
Youssou N'dour amehusika na maswala ya kibinadamu kwa siku nyingi na pia ni balozi wa shirika la umoja wa matataifa kuhusu maswala ya watoto (UNICEF).

Mwandishi wa BBC mjini Dakar, Thomas Fessy, anasema hatua ya bwana Youssou N'dour kutangaza kuwa atawania kiti cha urais, haijawashangaza wengi. Hii ni kufuatia tangazo alilotoa mwisho wa mwaka uliopita kuwa atajitosa katika ulingo wa kisiasa.
Katika hotuba iliyopeperushwa kupitia kituo chake cha redio na televisheni, mwanamuziki huyo amesema atapunguza matumizi ya serikali na kuahidi kuzalisha chakula na umeme kwa wote iwapo atachaguliwa kuwa rais wa Senegal.
''kuwa rais ni kazi sio taaluma''
Youssou N'dour anakubali kuwa yeye sio msomi lakini anaelezea wadhifa wa rais kama ''kazi na sio taaluma''.
Youssou N'dour alikuwa rafiki wa karibu wa rais Abdoulaye Wade, lakini baada ya Wade kutangaza nia ya kuwania kiti cha urais kwa muhula wa tatu, aligeuka na kuwa mpinzani wake mkuu.
Lakini haitakuwa kazi rahisi kwa Bw. Youssou Ndour kuwabadili maelfu ya wafuasi wake wa muziki kumpigia kura.
Aidha, Youssou N'dour amewahi kuwashutumu viongozi wa nchi za Afrika kuhusu jinsi walivyoshughulikia janga la njaa nchini Somalia.

Punguza Matumizi ya Posho SIYO Matumizi ya Reli, Barabara, Elimu na Afya - Zitto Kabwe



Waziri Kivuli Fedha na Uchumi, Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni (NKUB) na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Mhe. Kabwe Zuberi Zitto.
Mwezi Disemba mwaka 2011 Waziri wa Fedha na Uchumi alimwandikia barua Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Fedha Duniani (IMF) kumwahidi mambo yepi Serikali ya Tanzania itafanya ili kurekebisha Bajeti yake. Utaratibu huu hufanyika kila mwaka kupitia mpango unaoitwa ‘Policy Support Instrument (PSI). Katika barua hiyo Waziri wa Fedha wa Tanzania ameahidi kwamba Serikali itafanya juhudi kupunguza matumizi ili kuweza kupunguza uwiano wa nakisi ya Bajeti na Pato la Taifa (fiscal deficit to GDP ratio) kutoka asilimia 7.2 mpaka asilimia 6.6 ya Pato la Taifa.
Waziri wa Fedha na Uchumi ameiambia IMF kwamba ifikapo mwisho wa Mwezi Disemba mwaka 2011 (wiki mbili zilizopita) Baraza la Mawaziri la Tanzania limefikia maamuzi ya kupunguza nakisi ya Bajeti kwa kiwango kilichotajwa. Maeneo yanayotajwa ni Pamoja na Miradi ya Maendeleo ambapo jumla ya miradi yenye thamani ya Tshs 157bn itakatwa. Waziri
wa Fedha ametaja miradi hiyo katika Ukarabati na Ujenzi wa Miundombinu.
Kambi ya Upinzani Bungeni inapinga kuondolewa kwa miradi ya maendeleo ili kupunguza matumizi ya Serikali. Kimsingi wakati kama huu ambapo hali ya uchumi ni mbaya na vijana wengi vijijini na mijini hawana ajira tunasisitiza umuhimu wa kutumia zaidi kwenye miradi ya maendeleo.

Punguza matumizi ya kawaida
Kambi ya Upinzani Bungeni inarejea wito wake kwa Serikali kupunguza matumizi ya kawaida ili kupata fedha za kutosha kwa ajili ya maendeleo. Haiwezekani kamwe tukawa Taifa huru iwapo miradi yetu yote ya maendeleo inafadhiliwa na wahisani. Kiwango kidogo tulichokiweka katika Bajeti ya mwaka huu ndicho hicho sasa kinakatwa na hivyo miradi yote ya maendeleo kubakia kwa wahisani ama kwa mikopo au misaada.

Kiwango cha Tshs 203bn sawa na 0.5% ya Pato la Taifa ambacho Serikali imeahidi kupunguza ni kidogo mno na kinalenga kuumiza watumishi wa kada ya chini ya Serikali na sio viongozi wakubwa. Bajeti ya Mafunzo inayoenda kukatwa itaumiza Manesi na Walimu au watumishi wanaoongeza ujuzi ili kuboresha kazi zao. Serikali ikate matumizi yote yasiyo ya lazima na hasa posho (360bn), ipunguze matumizi ya magari na yale yasiyo na uhitaji yapigwe mnada na viongozi wote isipokuwa Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Spika na Jaji Mkuu washushwe madaraja ya kusafiria kwenye ndege. Safari zote ambazo hazina mahusiano na miradi ya maendeleo zipigwe marufuku kwa muda wote wa miezi sita ya Bajeti iliyobakia.
Serikali ihakikishe matumizi katika Sekta ya Elimu na Afya hayakatwi kabisa ili kuhakikisha tunalinda mafanikio kiduchu ya upanuzi wa sekta hizi na kuongeza uwezo wa Serikali kutoa huduma bora kwa wananchi hasa wa vijijini.

Matumizi ya Maendeleo yasiguswe, yaongezwe
Tayari imeonekana kwamba katika kipindi chote cha nusu ya Bajeti Halmashauri za Wilaya hazijapata fedha za maendeleo. Mfano Halmashauri ya Wilaya Kigoma imepata asilimia 0.3 tu ya Bajeti ya Maendeleo ilhali Halmashauri ya Mji wa Mpanda imepata asilimia 4 tu. Ni dhahiri miradi ya maendeleo kwa maeneo mengi ya vijijini itakwama kwani ni wazi kabisa kwamba Halmashauri hazipati fedha zote za Bajeti ya Maendeleo. Serikali itambue kwamba miradi ya maendeleo sio anasa bali ndio vyanzo vya baadaye vya mapato ya serikali. Miradi ya maendeleo hutoa ajira kwa wananchi na hivyo kuwapunguzia umasikini wa kipato. Jumla ya Tshs 157bn zinazotakiwa kukatwa zisikatwe bali ziongezwe ili kupata fedha za kurekebisha miundombinu kama Reli ya Kati.Kwa mfano Reli ya Kati inahitaji Tshs 200bn katika kipindi cha miaka 3 ili iweze kusafirisha mizigo tani 1.5m kwa mwaka kila siku na kuzalisha faida.

Ongeza Mapato ya Ndani
Inashangaza kwamba katika mpango wa Serikali kupunguza nakisi ya Bajeti mkazo umewekwa kwenye kuondoa miradi ya maendeleo badala ya kuongeza mapato. Nakisi hupunguzwa ama kwa kupunguza matumizi au kwa kuongeza Mapato. Serikali katika Taarifa yake kwa IMF imeibua njia moja tu ya kuongeza mapato, kodi ya mapato kutoka Kampuni ya Geita Goldmine. Huu ni uvivu wa kufikiri.

Serikali imeambiwa mara kadhaa suala la kuanza kutumika kwa sheria mpya ya madini kwa Kampuni za Madini zilizokuwapo. Makusanyo ya Mrahaba peke yake kwa sheria mpya, kiwango kipya na kanuni mpya ya kukokotoa ingeongeza mrahaba mpaka Tshs 203bn kutoka Tshs 99bn za sasa. Kwanini Serikali ianvuta miguu katika kutekeleza hili? Waziri wa Nishati na Madini aliahidi Bungeni kwamba mazungumzo na Kampuni za Madini yanaisha Mwezi Septemba. Mbona Serikali imekuwa BUBU katika hili?
Serikali iliahidi kuangalia suala la mauzo ya mali za makampuni zilizoko Tanzania na kodi ambayo tunapaswa kukusanya, Serikali imekuwa kimya kabisa katika suala hili. Marekebisho ya Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa kuondoa msamaha kwenye ‘deemed capital goods yangeongeza mapato ya Serikali kwa kiwango kikubwa na kupunguza mzigo wa
misamaha ya Kodi.

Uwajibikaji kwa Bunge
Inashangaza zaidi kwamba sasa imekuwa ni mtindo kwa Serikali kutoa ‘commitments’ muhimu za kibajeti kwa Shirika la IMF badala ya wananchi kupitia Bunge. Bunge limepitisha Bajeti, mapitio yeyote ya Bajeti yanapaswa kuidhinishwa na Bunge. Bila kufanya hivyo maana ya Bunge kupitisha Bajeti inakuwa haina mantiki na uhuru wa Taifa letu unakuwa haupo kwetu.

Umuhimu wa Bunge kutunga haraka Sheria ya Ofisi ya Bajeti ya Bunge (Parliamentary Budget Act) sasa unaonekana waziwazi. Muswada umewasilishwa Bungeni na Wabunge binafsi kutaka kuundwa kwa mfumo wa kuisimamia Serikali katika Bajeti. Ofisi ya Spika wa Bunge ihakikishe muswada huu unachapishwa katika Gazeti la Serikali mara moja ili usomwe kwa mara ya kwanza katika mkutano wa Sita wa Bunge na kutungwa kuwa sheria katika mkutano wa Saba.

Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali ilete mpango wa kupunguza matumizi Bungeni ili ujadiliwe na kuidhinishwa na Bunge kabla ya kuanza kutumika. Vinginevyo Mpango wa Serikali kwa IMF utakuwa ni kudharau wananchi na kuuza uhuru wetu kwa Shirika la Fedha la Kimataifa. Mwalimu Nyerere aliwahi kusema mwishoni mwa miaka ya Sabini ‘toka lini Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) limekuwa Wizara ya Fedha ya Kimataifa (International Ministry of Finance)?’

Gaddafi dikteta mwenye mafanikio makubwa, wosia wake waanikwa duniani



SIKU chache baada ya  kuuawa kwa kiongozi wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi, walibya na dunia kwa ujumla imeingia katika mitizamo tofauti kuhusu kiongozi huyo huku wengi wakikumbuka mafanikio aliyoleta kwa taifa hilo tofauti na viongozi wengine waliong’olewa kwa udikteta.Baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikimtangaza na kutafuta namna zote za kujenga picha ya udikteta bila kuangalia upande wa pili wa Libya iliyooachwa  na Gaddafi.


Baadhi ya mambo ambayo yamekuwa yakizungumziwa ni iwapo Libya ya sasa itaweza kuneemeka na kile ambacho ilikuwa ikipata kutoka kwa kiongozi huyo, ambaye  hivi karibuni  aliuawa na wapinzani wake.


Gaddafi, tofauti na viongozi wengine waliowahi kutajwa kuwa madikteta  duniani,  ana mengi ya kukumbukwa na kusifiwa kwayo.Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa na kiuongozi wamekuwa wakieleza kusikitishwa kwao na kutotambua aina ya demokrasia ambayo baadhi ya watu wa Libya wanaililia kwa sasa na iwapo itaboresha au kuharibu kabisa maisha yao.


Hii inawekwa wazi kwamba  pamoja na kwamba Gaddafi ametumia fedha nyingi za Libya katika masuala binafsi,  lakini je, kwa wastani Libya ni maskini? Wapo viongozi waliozitumia nchi zao na kuziharibu kabisa, Gaddafi aliwahi kuifilisi Libya?


Haya ni baadhi ya mambo ambayo Gaddafi  aliyasimamia na kuyatekeleza katika utawala wake wa miaka 42 kwa Libya.Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na tovuti za mawasiliano za Libya na Zimbabwe zimeeleza kuwa nchini Libya hakuna mwananchi aliyewahi kulipa bili ya umeme, umeme ulikuwa bure kwa raia wake wote.


Hakukuwa na riba katika mikopo, benki zote Libya zilikuwa chini ya Serikali,  mikopo ilitolewa kwa wananchi bila riba ya kiasi chochote .
Taarifa hizo zikafafanua kuwa makazi ni haki ya msingi nchini Libya, Gaddafi aliwahi kusisitiza kwamba wazazi wake hawawezi kupata makazi hadi kila raia apate makazi. Baba wa Gaddafi alifariki dunia wakati yeye, mama yake wakiwa wanaishi katika hema.


Wanandoa wote wapya nchini humo walipata Dola 50,000 kwa Serikali kwa ajili ya kununua makazi yao kuwasaidia kuanzisha familia mpya.Elimu na huduma za  kiafya vilitolewa bure. Wakati Gaddafi nachukua nchi  asilimia ya waliokuwa na elimu ilikuwa 25, kwa sasa inafikia  83.
Kwa waliotaka kuwa wakulima, walipewa ardhi bure, nyumba katika shamba lao, vifaa, mbegu na mifugo kwa ajili ya kuanzisha miradi.Iwapo kuna waliokuwa hawawezi kupata huduma za elimu na afya wanazostahili, Serikali iliwalipia kwa ajili ya kuzipata nje ya nchi, hizi hazikuwa bure, walitakiwa kuchangia, walipata Dola2,300 kwa mwezi kwa ajili ya makazi na usafiri.


Kwa waliokuwa wakitaka kununua magari,  Serikali ililipia kwa asilimia 50 ya bei. Bei ya petroli ilikuwa karibu na bure, lita ililipiwa kwa Dola 0.4.
Libya haidaiwi nje, pia ina akiba inayofikia Dola150 bilioni nje ambayo kwa sasa imezuiliwa.Kwa waliomaliza vyuo,  Serikali iliwapatia posho sawa na mshahara wa maofisa hadi watakapopata ajira yenye uhakika. Sehemu ya mauzo ya mafuta ya Libya iliwekwa moja kwa moja kwenye akaunti ya raia wake.


Kila mwanamke aliyejifungua alipata posho ya Dola5000, mikate 40 iliuzwa kwa dola0.15,  asilimia 25 wa Walibya, wana shahada ya chuo kikuu.Kama hiyo haitoshi taarifa hizo zimeeleza kuwa alisimamia mradi mkubwa kabisa wa umwagiliaji, uliopewa jina la Great Man-made River, kuhakikisha maji yanakuwepo kwenye maeneo yote ya nchi yenye jangwa.


Wakati wa vikwazo kwa Serikali yake miaka ya 1980, Libya ilikuwa miongoni mwa nchi tajiri kabisa kwa msingi wa pato la ndani, ikwa na kiwango cha juu cha maisha kuliko Japan. Ilikuwa ni nchi tajiri kuliko zote kabla ya vuguvugu la mapinduzi.
Wastani wa kiwango cha maisha kwa pato la kichwa ni Dola11,314 . Gaddafi amewahi kutumia fedha nyingi kwa ajili ya safari zake na miradi yake, lakini amefanya mabo makubwa ambayo hakuna dikteta aliyewahi kuyafanya kwa watu wake. Alirejesha pato kwa watu wake, aliwajali.


          Wosia wa Gaddafi kabla ya kifo
Katika wosia wake, Kanali Gaddafi aliwaasa wafuasi wanaomuunga mkono kuendelea kupambana.
Alielezea msimamo wake kuwa amechagua kupambana hadi hatua ya mwisho na kufia katika ardhi ya Libya kuliko kuchagua njia nyepesi, ambayo kwa mtizamo wake,  ni kitendo cha kujidhalilisha kisichokuwa na heshima, kukimbilia uhamishoni nje ya nchi yake, ambapo tayari alishapata ahadi nyingi za ulinzi.


Katika lugha ya Kiingereza, waraka wake wa wosia umetafsiriwa ukisomeka: “Hii ni hiyari yangu. Mimi Muammar bin Mohammad bin Abdussalam bin Humayd bin Abu Manyar bin Humayd bin Nayil al Fuhsi Gaddafi, ninaapa kwamba hakuna Mungu mwingine zaidi ya Allah na Muhammad ni Mtume wake, amani iko kwake. Ninaahidi nitakufa nikiwa Muislamu.


 “Iwapo nitauawa, nitapenda kuzikwa kwa mujibu wa taratibu za kiislamu, nikiwa nimevaa mavazi nitakayokuwa nimevaa wakati kifo change kikitokea, bila mwili wangu kuoshwa, katika makaburi ya Sirte, jirani na familia na jamaa zangu.


“Nitapenda kwamba familia yangu, hasa wanawake na watoto, watunzwe vyema baada ya kifo changu. Watu wa Libya wana wajibu wa kulinda wasifu, mafanikio, historia na heshima ya waasisi na mashujaa wake.


“Watu wa Libya hawatakiwi kupuuza kujitapa na lazima wawe  watu huru wa kuthaminiwa. Ninawataka wale wanaoniunga mkono kuendelea kupambana, kuwakabili wote wanaosimama kutoka nje dhidi ya Libya, leo, kesho na siku zote.


 “Hata kama hatutashinda mapema, tutatoa funzo kwa vizazi vyetu vijavyo, kwamba kuchagua kulinda utaifa ni heshima na kuliuza ni uasi mkubwa ambao historia haitausahau milele, pamoja na juhudi za wengine kuwaeleza kinyume cha hayo”.
 Msimamo wa Serikali ya Mpito ya Libya
Mustafa Abdul Jalil Kiongozi wa Baraza la Mpito la Libya alisema juzi kwamba sheria za Kiislamu zitakuwa msingi muhimu wa utungaji sheria nchini Libya.


Akizungumza katika mji wa Benghazi katika sherehe za kutangaza kukombolewa kwa nchi hiyo kutoka mikononi mwa utawala wa Gaddafi, Abdul Jalil alisema kuwa Libya ikiwa ni nchi ya Kiislamu itatunga sheria zake kutokana na mafundisho ya Kiislamu na kwa msingi huo sheria zote zilizokuwa zikitumiwa na utawala wa Gaddafi kupiga vita Uislamu zitafutwa.


Alizishukuru Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, Umoja wa Mataifa na Umoja wa Ulaya kwa kuisaidia Libya kumwondoa madarakani Gaddafi.


Abdul Jalil pia alizungumzia mipango ya kuanzisha Benki za Kiislamu nchini Libya hivi karibuni na kuongeza kuwa benki hizo hazitakuwa zikichukua wala kutoa riba na kwamba zitatekeleza shughuli zao kwa msingi wa mafundisho ya Kiislamu.


Alisema kwamba mapinduzi ya wananchi wa Libya yalianza kwa amani, lakini yalikabiliwa na vitendo vya mabavu na nguvu kutoka kwa utawala wa dikteta Gaddafi.

Mh Magufuli atangaza neema Kigamboni


SERIKALI jana ilitiliana saini na Kampuni ya China Railways Construction Engineers Group kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Daraja la Kigamboni mwezi huu.

Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa kampuni hiyo kwa kushirikiana na Kampuni ya China Major Bridge, ilishinda zabuni ya kujenga daraja hilo katika kipindi cha miaka mitatu, baada ya Kampuni ya Arab Consulting Engineers kumaliza kazi ya upembuzi yakinifu.

Dk Magufuli alisema daraja hilo la Kigamboni linatarajiwa kugharimu Sh214.6 bilioni, fedha ambazo Serikali itachangia asilimia 40 na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), asilimia 60.

Akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya kutia msaini mkataba huo, Dk Magufuli alisema lengo la Serikali kujenga Daraja la Kigamboni ambalo ujenzi wake unaanza mwezi huu ni kuleta maendeleo na kuinua uchumi hivyo kuwataka wananchi kushirikiana nayo ili kuhakikisha kuwa azma hiyo inatekelezwa kwa vitendo na si kuleta maneno.

Alisema NSSF ilitangaza zabuni ya ujenzi wa daraja hilo na kampuni 15 zilijitokeza, saba kati ya hizo ndizo zilizoingia kwenye kinyang’anyiro hicho.

Daraja hilo litahusisha ujenzi wa mita 680, njia sita za lami kwa umbali wa kilomita 1.0 kwa upande wa Kurasini na njia sita za lami kwa umbali wa kilomita 1.5 upande wa Kigamboni.

“Wananachi wa Kigamboni na maeneo mbalimbali wataweza kutumia daraja hilo kwa ajili ya kurahisisha shughuli za maendeleo. Tunapaswa tushirikiane ili kuhakikisha kuwa daraja hilo linakamilika kwa muda uliopangwa,” alisema.

Alisema kwa upande wa kusini, daraja hilo litaungana na Barabara ya Mandela kuelekea Tazara wakati upande mwingine utaungana na Barabara ya Kurasini kuelekea Kamata na zote kwa pamoja zitafanyiwa matengenezo ili kupunguza msongamano wa magari.

Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk Ramadhan Dau alisema tathmini ya awali ya ujenzi wa daraja hilo ilianza mwaka 1977... “Ilipofika mwaka 1991, Serikali iliendelea na upembuzi yakinifu chini ya Kampuni ya Gauff ya Ujerumani ambayo ilionyesha gharama za ujenzi huo kuwa ni zaidi ya Dola 47 milioni.”

“Kutokana na ukosefu wa fedha ujenzi huo ulishindikana. Mwaka 2002, NSSF walianza mazungumzo mapya na kufanya upembuzi yakinifu mwaka 2003 na ilipofika mwaka 2005, shirika hilo liliingia mkataba na kampuni ya Arab Consulting Engineers ya Misri kwa ajili ya upembuzi wa kina. Kampuni hiyo ilishauri kuwa mradi usingeweza kuwa na faida kibiashara mpaka Serikali itoe ruzuku.” 

Apiga vijembe
Akizungumza katika hafla ya kutiliana saini mkataba huo, Waziri Magufuli aliwapiga vijembe wanasiasa wanaomshambulia kwa uamuzi wake wa kuongeza bei ya Kivuko cha Kigamboni akisema: “Maendeleo ya nchi hayaangalii itikadi ya chama, iwe CCM, Chadema, CUF na vyama vingine.”



Alisema kila mmoja ana jukumu la kuhakikisha kuwa wanashirikiana na Serikali ili kuleta maendeleo.
Alisema mambo ya siasa yanachangia kuongeza chuki, migongano na vurugu za hapa na pale, hivyo akasisitiza umuhimu kwa Watanzania kuyaepuka.

Waziri huyo alisema mkakati wa Serikali ni kutekeleza ahadi ilizoahidi wakati wa uchaguzi na si kulumbana wala kugombana.Aliwataka Watanzania kutambua kuwa siasa ni mambo ya mpito, lakini mwisho wa siku wataalamu wataendelea na shughuli zao kama kawaida.

“Ninawaomba wananchi waache mambo ya siasa ili kutoa nafasi kwa wataalamu kufanya kazi zao na si kuwaingilia kwa sababu siasa inapoteza muda na kurudisha nyuma maendeleo... jamii inapaswa kujifunza mambo hayo,” alisema Dk Magufuli.

Wanafunzi waliofutiwa matokeo ya Darasa la Saba kurudia mitihani

Mwalimu wa darasa la kwanza wa Shule ya Msingi Bungo iliyopo Manispaa ya Morogoro, Asinath Mshana akimwelekeza namna ya kuumba herufi mwanafunzi wa darasa la kwanza, Nesto Robert , shuleni hapo jana baada ya Shule za Msingi nchini kufunguliwa. 


SERIKALI imeamua kwamba watahiniwa 9,629 waliofutiwa matokeo ya mtihani wa darasa la saba uliofanyika mwaka jana baada ya kugundulika kufanya udanganyifu, warudie mtihani huo Septemba mwaka huu.


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo alisema kiwango cha wanafunzi waliofutiwa matokeo ni kikubwa na hiyo ndiyo sababu pekee iliyoisukuma Serikali kuwapa nafasi ya kurudia mtihani huo.  


Hata hivyo, alisema uamuzi huo unawahusu wanafunzi wale tu waliogundulika kuwa na majibu yenye mfanano usio wa kawaida na kwamba uamuzi huo hautawagusa wanafunzi 107 ambao walifutiwa matokeo yao baada ya kukutwa na majibu.


“Suala hili la majibu kufanana linaonekana limechangiwa zaidi na walimu… lakini pia wazazi wametoa maoni yao na Serikali imeona iwape nafasi nyingine ya kurudia mtihani huu.” 


 Alisema halmashauri kwa kushirikiana na shule zinatakiwa kuandaa utaratibu utakaowawezesha watahiniwa hao kujiandaa kimasomo  mpaka watakapofanya mtihani huo, huku akiagiza wanafunzi hao kujisajili Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) kabla ya 30 Januari, mwaka huu.  Alisema kwa shule zenye idadi ndogo ya wanafunzi waliofutiwa matokeo,  zinaweza kuwaruhusu kuhudhuria darasani pamoja na wanafunzi wa darasa la saba wa mwaka huu, huku zenye idadi kubwa ya wanafunzi akiziagiza kuandaa utaratibu wa kutoa masomo nyakati za jioni.  


Mulugo alisema watahiniwa hao watafanya mtihani huo sambamba na wenzao wa mwaka huu.  Desemba 14, mwaka jana, Serikali ilitangaza matokeo ya darasa la saba ambayo kati ya wanafunzi 983,545 waliofanya mtihani huo, 567,767 sawa na asilimia 58.28 walifaulu, huku ikifuta matokeo ya watahiniwa 9,736. 


Miongoni mwa waliofutiwa matokeo hayo, wanafunzi 94 walikamatwa na karatasi za majibu, wanne walibainika kuandikiwa majibu, tisa walibainika kukariri darasa kinyume na utaratibu na 9,629 walibainika kuwa na majibu yenye mfanano usio wa kawaida.  


Yaunda tume  Waziri huyo alisema Serikali imeunda tume chini ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na ile ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), kuchunguza chanzo cha udanganyifu  na  kutoa mapendekezo ya kudhibiti vitendo vya udanganyifu katika mitihani.  
Alisema taarifa ya uchunguzi wa tume hiyo itatolewa mwishoni mwa Aprili mwaka huu, huku akisema hatua kadhaa zinaendelea kuchukuliwa na mamlaka mbalimbali kwa wahusika.  “Watendaji au taasisi zitakazobainika kuhusika kwa namna yoyote katika udanganyifu zitachukuliwa hatua,” alisema na kuiomba jamii hususan wazazi kujiepusha na udanganyifu kwa kuwalea watoto katika misingi ya maadili, kujiamini na kujitegemea katika maisha.  


Ada shule binafsi  Akizungumzia viwango vikubwa vya ada vinavyotozwa  katika shule binafsi, Waziri Mulugo alisema suala hilo linafanyiwa kazi na Serikali ikiwa ni pamoja na kupitia kwa undani mfumo mzima wa ulipaji ada ili iweze kutoa uamuzi wa haki kwa pande zote.  


“Kuna shule za dini, binafsi na za jumuiya, zote zinatoza ada kulingana na gharama za ufundishaji. Zipo ambazo hufanya mafunzo kwa njia ya vitendo nje ya nchi… hii ni gharama pia ndiyo maana tunasema kuwa tunahitaji muda zaidi kulishughulikia hili,” alisema.  


Mitalaa  Waziri Mulugo amezionya shule zinazofundisha kwa kutumia mitalaa ya nchi nyingine. Alisema kama kuna haja ya kufanya hivyo, zinatakiwa kuwa na kibali cha Serikali.  


“Kuna shule moja ilikuwa Mwenge, niliifungia kwa kuwa ilikuwa ikifundisha wanafunzi kwa mtalaa wa nchi ya Kongo (DRC). Sasa kuna tetesi kuwa wamehamia eneo la Ubungo na wanaendelea kufundisha, nitakwenda mwenyewe kuhakikisha na kama ni kweli, wahusika watakamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya dola,” alisema.