Wednesday, January 11, 2012

IDARA YA UHAMIAJI YAKAMATA MTANDAO WA BIASHARA YA BINADAMU



Idara ya uhamiaji nchini Tanzania imeendesha msako maalumu na kufanikiwa kukamata mtandao unaojishughulisha na biashara haramu ya binadamu unaoongozwa na mtu aitwaye Ashok Nepal raia Bangladesh.
Naibu kamishna wa Uhamiaji, Bi. Grace Hokororo amesema kuwa katika operesheni hiyo jumla ya watu kumi na sita wamekamatwa wakiwemo raia kutoka nchi za Pakistani, Nepal na Kenya.
Kwa mujibu wa Bi. Hokororo, Ashok anatuhumiwa kuwaingiza chini isivyo halali watu hao na baadaye kuwatafutia viza kwenda nchini Afrika Kusini kwa malipo ya dola za Marekani elfu tano au dawa za kulevya zenye thamani hiyo hiyo ya fedha.

No comments:

Post a Comment