Wednesday, January 11, 2012

MWANAMKE AFA AKIJARIBU KUOKOA SIMU YAKE!!

Charlene Pickering



Mwanamama mmoja nchini Uingereza amekufa kwa kugogwa na treni ya mwendo kasi baada ya kuruka kwenye mabehewa ili kuiokoa simu yake.
Mwanamama huyo Charlene Pickering,mwenye miaka 23 alikuwa akigombana na mpenzi wake Daniel Pickett wakati alipoiangusha simu hiyo na kujigonga mara nyingi kabla kuangukia kwenye mabehewa.
Mpenzi wake Bw. Pickett alimuomba kurudi katika ghorofa walipokuwa wamesimama lakini ombi lake hilo lilichelewa sana baada ya mwanamke huyo kugongwa na treni ya mwendo aksi inayosafiri mita 60.
Bi. Pickering,anayetoka Magharibi mwa mji wa Molesey, Surrey, ametangazwa kufa katika ajali hiyo kufuatia tukio ilitokea kituo cha Wimbledon kusini magharibi mwa London.

No comments:

Post a Comment