Wednesday, January 11, 2012

MZEE KIPARA AFARIKI DUNIA!!


Hayati Mzee Kipara


Taarifa zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa mwigizaji mkongwe nchini Tanzania aliyewahi kutamba na kundi la Kaole Fundi Saidi maarufu kama Mzee Kipara amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Akithibitisha taarifa hizo mwigizaji mkongwe Swebe amesema mzee Kipara amefariki leo saa mbili asubuhi akiwa nyumbani Kwake Kigogo jijini Dar es salaam ambapo mpaka anatufikisha taarifa hizi Swebe ndiye aliyekuwa na maiti ya mzee Kipara ndani akifanya jitihada za kuipeleka maiti hiyo Muhimbili.



Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi,Ameen!

Habari kwa Hisani ya Zembwela na Michael Baruti. 

No comments:

Post a Comment